SIMON KITURURU- MAWAZONI

  • ASILIMIA kubwa ya kitu watu waitacho SALAMU,....

    Posted: March 15, 2010, 7:03 am by SIMON KITURURU
    ... labda sio SALAMU.:-(

    Swali:
    • Wakati unasalimia mtu unauhakika na kitu ufanyacho zaidi ya kuamini tu UFANYACHO ni kusalimia?

    • Unauhakika SALAMU ni nini ikiwa  KUTIKISA KICHWA, kusonya, KUPIGA MAGOTI, kukonyeza na mpaka sentensi ; ``Shikamoo MWAAALIMU!´´na....,....``Sema wee Msenge!´´ kuna watu ni SALAMU?
    Ndio,....... kunauwezekano WENGI wasalimiao MTU hawajawahi kufikiria SALAMU ni nini.:-(
    NI WAZO TU hili MKUU!JUMATATU NJEMA!
  • Wakati tunafikiria HISTORIA ya JINSI mtu anavyojifunza kuona AIBU kukaa uchi !

    Posted: March 15, 2010, 6:14 am by SIMON KITURURU
    [Tahadhari :WAZO limepinda na laweza lisikufunze kitu kama sio MFIKIRIAJI!:-(]

    Mtu akizaliwa kwa taratibu huanza kujifunza,...
    ..... MPAKA nini kiko  UCHI,....... na kwa kuigiliza hufikia mpaka kutafutia titi SIDILIA.
    Mwalimu mkubwa katika swala LA KUFICHA PIA mtu  ana-FUNZA,....
    ..... ni MACHO YA WATU na masura yao yageukavyo NAKUKUANGALIA VIBAYA wakati yanashuhudia unavyokatambuga  huku miguu iko SAA TISA KASOROBO wakati sio riadha UNAKIMBIA.:-(
    Macho ya watu hata kabla HUJAKEMEWA ubane miguu watu kwa bahati mbaya wasikuone NANIHII  ndio yanafunza,....
    ..... kuwa kuna vitu  onyesha MIJUSI na BATA  lakini sio WATU kama  heshima yako wataka kukuanayo ifanane na jinsi JAMII yako iaminicho ni heshima ukue vilivyo UKIISHIKILIA.:-(

    Swali:
    • Lakini si  unajua labda MACHONI mwa PAKA hakuna BINADAMU apendezaye UCHI?
    • Si unakumbuka ulizaliwa uchi na labda ulisha wahi kumnyea mgeni pia BILA AIBUB ingawa hilo hukumbuki?

    CHA kusikitisha ni kwamba,....
    .....BINADAMU kimchekeshacho utotoni kutokana na udhaifu WAKUJIFUNZA ,........ mpe muda waweza kumkuta HUYOHUYO kimwana UKUBWANI kilekile eti kinamfanya ANALIA.:-(


    Na LABDA binadamu badala ya kuona AIBU baada ya uchi  KUJIFUNZA,.....
    ... angeweza kustukia katika MWILI wa binadamu  labda UCHI ni  kipengele ambacho ukijua KUKABILIANA NACHO  kinakufundisha maisha kama hasa ukikumbuka kuwa UKIJISWAFI kipengele hutanuka na shughuli ya KUJISWAFI hata uchoke inahitaji kukumbukwa kwa KUACHA UVIVU kama wataka  kipengele kivutie na wataka MWILI mzima usinuke hata kama nia sio watu wasistukie  UNANUKIA.
    Na baada ya hilo la uchi  KUJIFUNZA,....
    .... waweza kugundua wewe kama BINADAMU hata YAKO DHAMIRA au tu AKILI kama tu uchi unahitaji KUISWAFI mara kwa mara hata kama UNASIKIA UVIVU ili  kuwa safi kama BINADAMU kiroho na KIMWILI  na HASA kama wataka YAKUZINGUAYO uyatoke baruti na kuyapa MKIA.


    Swali
    • AU?

    Na kunauwezekano,...
    ....KUONEA aibu kitu ni kitendo cha KUJIFUNZA,........ na wote wachezao MUZIKI na nguo wakifuatilia HISTORIA YA WACHEZA MUZIKI  wanaweza kugundua labda starehe halisi hata ya SINDIMBA ni kuicheza titi nje kwa kuwa labda vazi halisi la kuchezea muziki wala hata sio KIBWAYA bali ni kucheza uchi.:-(



    Swali:
    • Si unakumbuka kunibishia RUKSA?


    Lakini kuna waaminio kutokana na mafundisho ya DINI ZAO  kuwa EVA yule demu wa ADAMU kama baadhi ya VITABU vya BAADHI YA DINI VIDAIVYO  ndiye alianzisha mchezo wa kuona AIBU na kuficha uchi baada ya kula TUNDA alilopewa na MJANJA shetani ambalo alifanikiwa kumuonjesha ADAMU  akasikia tamu ndio mpaka akajistukia yuko UCHI.

    Na kama unaami HILO miye  SIKUBISHII  hasa kama umewahi KUFIKIRIA  jinsi ulivyojifunza kuwa na AIBU kukaa UCHI na kufikia hitimisho ni kosa la EVA ndio sababu unaficha uchi.:-(


    Na labda PIA  ni kweli ,...
    ....katika HISTORIA fupi ya binadamu CHA KUSIKITISHA  huwa inaambatanisha KUZALIWA uchi  na mwisho kufa na kuoza mpaka uchi.:-(


    SAMAHANI NAACHA WAZO MHESHIMIWA !:-(




    Hebu tu PAPA WEMBA apoze shughuli NA KURUDISHA USTAARABU hapa KIJIWENI  kwa ndude-YOLELE


    Au tu tubaki hapahapa KONGO Papa WEMBA asawazishe shughuli kwa kitu- SHOW ME THE WAY

  • Tamu ya KUJIDANGANYA,.....

    Posted: March 15, 2010, 4:37 am by SIMON KITURURU
    .... inaweza KUSABABISHA kuwezesha kila  UNACHOJISIKIA UKISEMA kukigeuza ni KWELI.:-(


    Swali:
    • Si unajua INASEMEKANA ukirudiarudia kudanganya WATU  KITU  unaweza kuanza kukiamini mwenyewe HICHO  KITU kuwa ni KWELI?
    • Si unajua siri ya kukabili  kutojisikia M-BAYA yenye mafanikio SANA inasemekana ni kujiaminisha mwenyewe KWA KUJIDANGANYA  kila mara ukijiangalia kwenye kioo kuwa WEWE MZURI?

    KUJIDANGANYA ni baabu kubwa,...... ndio maana kuna watu wengi INASEMEKANA wamefaulu mpaka KUFIKIA kuamini wataenda MBINGUNI kitu ambacho KWA MTU kunauwezekano  kikawaida na KIUDHAIFU WA KIBINADAMU  hawezi kufikia.:-(

    Swali:
    • Unauhakika IMANI sio MBINU ya kumsaidia MTU KUJIDANGANYA ndio maana aaminiye N'GOMBE, mbuyu, YESU, BUDDHA, Kikwete, OBAMA , BIBI TITI, SHEKHE YAHYA , Simon KITURURU , HAWALA,  BINAMU nyama ya HAMU, wote waaminicho kwa IMANI wanakigeuza UKWELI?
    NDIO,...
    ....kama wewe ni MTU kuna uwezekano  hicho ndicho KIPIGACHO KELELE kuwa unaweza KUDANGANYWA  .:-(
    Kwanza kama utasifiwa leo kuwa UMEPENDEZA labda ni UONGO.:-(

    NI WAZO TU HILI  MKUU WA KITENGO!
    Hebu twende MALI  ili Mama Toumani alete mtekenyo uitwao- Niemogo

  • wakati mtu ANAHISI ANAKUJUA labda ndio huwa rahisi kukutukania KIPENGELE CHA SIRI shenzi!:-(

    Posted: March 15, 2010, 4:26 am by SIMON KITURURU
    KUHISI nishai kwa kuwa WATU,........huchanganya HISIA  na ni nini ni KWELI.:-(
    NA kwa kuwa  kujua UKWELI ni shughuli na WATU ni wavivu kujishughulisha hasa na MAGUMU ya watu ,....... wapendayo kuyaamini  kirahisi hutokana na HISIA tu na labda hasa zile zimuunganishazo mtu na MAMBO YA AJABU KIMPINDO  au MAZURI KUPITA  KIASI kama SIO MABAYA KUPITA KIASI  yenye stori tamu ZITEKENYAZO HISIA KINAMNA  ingawa hayana UKWELI.:-(

    Swali:
    • Huwa unakumbuka kutofautisha unavyomuhisi ASKOFU au SHEKHE na halihalisi AMBAYO ndio  ukweli ambao unaweza kuwa HUYO ni MWIZI na malaya kwa mbaaali kitu kisichokuwa na uhusiano na wadhifa wake wa DINI UUHESHIMUO ufanyao UMHISI na yeye  vingine ?

    • Si unakumbuka kama UNAHISI tendo hilo linatonya kuwa kuna kitu HUNA UHAKIKA kwa kuwa HUJADAKA MTU AKISHUGHULIKA  na labda ndio kisa bado KUNA MTU  hajamfukuza kazi hausigeli LEO  ingawa anawasiwasi ni kiburudisho cha mmewe akiwa kazini?

    • Unauhakika HUWA unajua UKWELI au hata uwaitao MAFISADI ni kwa HISIA tu ?



    Na kwa KUHISI kuna wengi wanahukumu watu na VITU ,...
    .... ingawa UKWELI wenyewe labda  ni kweli BIKIRA Maria baada ya kujifungua alibakia bikira  HATA KAMA hisia zako ZINAPINGA na TANZANIA kweli ina amani  kama tu isivyo UKWELI.:-(
    Swali:
    • Unabisha?
    • Hivi hapa kwenye BLOGU huwa unahisi UNANIELEWA au unajua HUNIELEWI?


    NDIO,....
    ....labda sio hisia zako tu,....... kuna uwezekano UKWELI wenyewe nilichoandika ni UJINGA hapa.:-(

    Lakini SI UNAJUA kama unahisi una NJAA ,....
    ...kumbuka wewe hunanjaa KIKWELI  kwa kuwa kwa kawaida MWENYE NJAA hujua  na sio HUHISI kuwa ANA NJAA.:-(

    NIMEACHA!:-(





    Hebu twende ETHIOPIA ili TEDDY AFRO arudishe mambo mpwito kwa ndude- AYNE



    Au tu TEDDY AFRO atulize manyanga kwa kitu-MUZIQA HIWETE



    Au tusiondoke ETHIOPIA bila TEDDY AFRO kumwaga tena ndude-JAH


Blah blah blah

Fish cakes

Alas a fish cake.

Yet more fish cakes

Guess what ... yeah ... fish cakes.

The end of the fish cakes


Kenyan Blogs