SIMON KITURURU- MAWAZONI
-
MTOTO MZURI labda JAMBA tu usiahirishe,...
Posted: February 27, 2010, 7:20 pm by SIMON KITURURU
.... kwa kuwa kama umewahi KUBANWA na kijambo,......... wajua JUHUDI na JEURI za waliobanwa kijambo WASIOJAMBA HADHARANI sana sana ni za kusogeza MUDA tu WAKUJAMBA iliusisikie wakijamba ,....... na AFYA YA KIJAMBO CHAO kwa bahati mbaya bado huwa iko PALEPALE.:-(
Na MTOTO MZURI labda NI BUSARA PIA kijambo usilazimishe,...
....kwa kuwa ALAZIMISHAYE KUJAMBA anaweza akafanikiwa KUHARISHA PIA juu ya kijambo hasa KWA KUWA nukta ya kutolea uharisho NI ILEILE ambayo ukizidisha JUHUDI hewa itaongezewa CHEMBECHEMBE NA ROJO katika MTOKO utumiao tobo ambalo wengi hutambua kuwa HUWA linanunia shughuli sehemu mbali mbali lakini katika tundu lililopo PALEPALE.:-(
Swali:- Unafikiri kwa kuahirisha UJUACHO utafanya WATU WENGINE wasipokuwepo kuna badili kuwa utakachofanya ni KILEKILE?
- Unafikiri ukidokoa MBOGA bila kuonekana kitendo chako hugeuka kuwa NI kuonja MBOGA?
NDIO,...... moja ya BUSARA za BINADAMU ni kuficha vitu vijulikanavyo SIO SIRI na kuwageuza wavifanyao HADHARANI mahawayani ingawa LABDA uhawayani WENYEWE WENYE TAKO KUBWA ni ule UTU na HESHIMA ZA MTU zenye misingi ijengwayo kwa kuwa tu NI HESHIMA eti MJUACHO ANAFANYA kafanya SIRI.:-(
NIMEACHA!
Tahadhari: MHESHIMIWA hii taralila HAINA uhusiano na KUJAMBA!:-(
Hebu tubadili wazo HASA kwa kuwa kwenye taralila isiyona uhusiano na KUJAMBA inaneno JAMBA lisilo la HESHIMA kwa BAADHI YA WAUNGWANA WAJAMBAO kwa kuwaachia En Vogue wadai- My Lovin' (Never Gonna Get It)
Salt N Pepa wazungumzie - Shoop
Au tu NAUGHTY by NATURE warudie tu.- FEEL me FLOW
-
Kwa kuwa , ...KUWA na DHAMBI ni tofauti na JINSI ya kujisikia una DHAMBI!
Posted: February 27, 2010, 5:28 pm by SIMON KITURURU
[ Tahadhari: JIHADHARI na WAZO hasa kama ULIVYO na unavyojisikia UNAFIKIRI ni sawasawa!:-(]
Kuna UWEZEKANO kabisaaa...
...kuwa MASIKINI ni tajiri kama hujamfundisha MHUSIKA jinsi ya kuusikilizia UMASIKINI!:-(
MATATIZO ya UMASIKINI ni MATATIZO tu kawaida ,...... na LABDA mpaka uyaoanishe tu na UMASIKINI ndio matatizo AMBAYO NI MATATIZO kutokunya KIKAWAIDA kwenye jedwali la MATATIZO kuna ambayo utayaambatanisha na SEKSHENI a.k.a kipengele cha MATATIZO yaletwayo na kibano cha UMASIKINI na kuyafanya kuwa MATATIZO HAYO ni MATATIZO YA UMASIKINI.:-(
Samahani,....
..... nimekumbuka , NIA na MADHUMUNI ya taralila hii ni kuongelea DHAMBI.:-(
DHAMBI ,...
....ni FIKIRA aliyokuwanayo MTU hasa baada ya TENDO,...
.... kwa kuwa DHAMBI inaweza ikawa ni TENDO LA NDOA kabla HUJAFIKIRIA na kulioanisha kifikira na UZINZI.:-(
Kwahiyo ;...
...DHAMBI usiishangae kama ni tamu!
Na labda unajua hata kama naheshimu kwamba HUTAKIRI,...
.... wala DHAMBI hainauhusiano na UCHUNGU ingawa KIFIKIRA neno dhambi linamchezo wakufanya hata utamu wa ULICHODOKOA ufikiriacho ni KISAFI KIFISADI katika TAMU yake YA MSHIKAKI ukahisi KWAKE kunyunyiziwa chembechembe za kamasi la MPIGA CHAFYA ambalo husababisha utamu wa peremende usikilizwa kwa mikwaruzo ya ujuaji labda moja ya ifanyayo PEREMENDE tamu ni kamasi.:-(!
Swali:- AU?
Ndio,.......DHAMBI ingekuwa MCHICHA,.......kuna watu tungejaza TENGA!:-(
Ila kwa jinsi DHAMBiI ilivyokuwa NYOKO,...
.... ahubiriye DHAMBI mara karibu zote ndiye aliyekuwa na TAFSIRI FULANI ya uhakika kwake YA DHAMBI ,.......kitu kifanyacho awe miongoni mwa WATU ambao kwa uhakika wanajua wafanyavyo ni DHAMBI.:-(
Ndio ,...
...jinsi yako YA kufanya DHAMBI yaweza kuathiriwa na STAILI yako ya unavyoisikilizia DHAMBI.
Na kwa kuifikiria dhambi,...waweza kustukia katika dunia ya WENYE DHAMBI, watu wengi wanakustukia WEYE ni MWENYE DHAMBI kwa kuwa tu NI KWELI katika wafunikao kwa GWAGURO ,......WEYE unaikalia uchi na kuionyesha masharubu ya chini DHAMBI .:-(
Tukiacha MZAHA ;....Swali:- Unauhakika DHAMBI ni nini?
- Unafikiri UMASIKINI USIKILIZIWAVYO kama tu DHAMBI , unauhakika MASIKINI ni muda gani HUWA anajisikia MASIKINI?
- Unauhakika TAJIRI anajisikia tajiri wakati anakunya?
- Unafikiri wewe kama ni MKRISTO ambaye kwako ruksa ni kuonjeshwa kidude kimoja tu NA MKE WAKO WA NDOA huwa unaelewaje na KUIGEUZA NI DHAMBI ya MUISLAMU ambaye kwake SIO DHAMBI ,- ile ya KUONJESHWA VIDUDE VINNE kutoka kwa WAKE WANNE WA NDOA awawezao kuwapa huduma WAJISIKIE NI WAKE WA MTU wapatao matekenyo yote ya NDOA kwa maadili ya KIISLAMU?
- Unafikiri dhambi yako ya UZINZI inafanana na dhambi ufikiriayo ni HIYO HIYO kwa mwingine YULE aliyedakwa UGONI na wewe ambaye hafikirii kama WEWE?
- Unafikiri kuna MTU anajisikia ana DHAMBI kama alivyo na DHAMBI?
NI HILO TU!JARIBU TU kukumbuka ni TAFAKURI tu hii MHESHIMIWA na KUNAUWEZEKANO kama WAZO HILI limevalishwa chupi , basi chupi INATOBO!:-(
Hebu ANDREW SAMUEL alainishe na kubadili HALI YA HEWA KIJIWENI kwa ndude-Pinacolada
Maxi Priest abadili zaidi kwa ndude-Close to U
Au tu MAXI Priest amalizie tu kwa ndude-Just a little bit longer
-
WAKATI kunauwezekano UFIKIRIACHO ni FIKIRA tu!:-(
Posted: February 27, 2010, 5:12 am by SIMON KITURURU
NDIO,...... ..labda kuna WATU unafikiri,.......wanakufikiria UNAVYOFIKIRIA unavyofikiriwa.:-(
Swali:- Lakini unafikiri WATU wanakufikiriaje WEYE?
Ndio,...
....kuna PADRI katika fikira haoanishwi na NYEGE YA DHAMBI,....
.....kwa kuwa ni kweli ndani ya siku yake HUHUSIANISHWA na mtekenyo ulazimishao baadhi ya watu WACHUMBIE malaya ambaye NI KWELI afanyacho kwa kawaida ndani ya siku SIO DHAMBI wala UMALAYA.:-(
Swali:- Unafikiri MALAYA afanyacho ni UMALAYA siku nzima?
- Si unakumbuka wewe sio UNAVYOFIKIRIWA kwa kuwa kitu halisi sio FIKIRA?
NIMEACHA tafakuri hii!Kumbuka hili ni WAZO TU MKUU na labda si AJABU kujaribu KUPATA POINTI ya hoja YAKE MHESHIMIWA!:-(
Hebu Macy Gray abadili kwa -I TRY
Au tu Corinne Bailey Rae abadili kidogo zaidi kwa -I'd Like To
Blah blah blah
Fish cakes
Alas a fish cake.
Yet more fish cakes
Guess what ... yeah ... fish cakes.
The end of the fish cakes