SIMON KITURURU- MAWAZONI

  • UJUMBE MZURI ni kama UGALI,saa nyingine ni MPAKA uwe na MBOGA tamu ya kusukumizia TONGE ndio kitaeleweka!:-(

    Posted: February 22, 2010, 1:19 pm by SIMON KITURURU



    UJUMBE MZURI labda hautoshi kwa kuwa tu ni UJUMBE MZURI,...... ukizingatia walengwao  wanaweza wasiupokee USIPOSINDIKIZWA na kulainishwa na  NJIA ambazo walengwa hawafikirii ni MBAYA.:-(
    Swali:
    • Si unajua kuna watu bila TAARABU  mahubiri yako YENYE UJUMBE MZURI WA BUSARA kuhusu mapenzi hawatayaelewa?


     UJUMBE MZURI ,..
    ....kwa kawaida hausikilizwi  kwenye WIMBO MBAYA.:-(

    Na kuna wengi WASIKILIZAO matusi  vizuri,...
    ... ambao ni UJUMBE WASIOUPENDA  kwa kuwa tu wanapenda mrindimo wa muziki  AMBAO KWAO ni  wenye UJUMBE MBAYA .:-(

    Ndio,.......kuna wamsikilizao pia  MTU vizuri ,....... kisa WANALAZIMIKA kuwa watulivu nakusikiliza  KWA KUWA wanatishwa na sura lake BAYA.:-(


    Swali:

    • AU?
    • Si unakumbuka ugali  unaweza usiliwe kama hauletwi mezani na MBOGA tamu? 
    • Si unakumbuka UGALI mbaya unaweza kuliwa kama mboga tamu?
    • Kwani wewe hakuna wimbo uupendao ambao unajua UJUMBE WAKE NI NYOKO lakini hata hivyo unaurudiarudia NA MPAKA KUUKARIRI  WIMBO huo  wenye UJUMBE MBAYA KWAKO na kwa  MATOTO YAKO huku ukitingisha bichwa lako kisa mirindimo ya MUZIKI na SAUTI ya muimbaji  vinakukuna nanihii kunako?


    Ndio,.......TATIZO ni ,......ujumbe MZURI katika hata HOTUBA ,....... labda inahitaji SURA fulani au tu SAUTI fulani  ili walengwao na UJUMBE wasikilize UJUMBE bila kushikiwa VIBOKO.:-(

    Swali:

    • Si nasikia kuna wamsikilizao Barrack Obama  Marekani kisa wanapenda sauti na WANAOMSIKILIZA Rais KIKWETE Tanzania kisa wanampenda sura?
    • Si unakumbuka kuna sababu  si kila mtu  WEWE unamsikiliza ?
    • Si unajua kuna uwezekano majibu ya matatizo yako ulishapewa ila hukuyasikia kisa hukupenda wimbo au sura tu ya MTOA suluhisho?
    • Si unajua upendaye kumsikiliza unaweza kunogewa kufuatilia azungumziavyo jinsi ya kutatua matatizo ya kujisaidia kwa bata kuhitajivyo bata wavalishwe chupi kuliko USIYEPENDA kumsikiliza akizungumzia jinsi ya KUTATUA matatizo yako?




    Ndio,..... labda  HATA MAANDISHI  usiyopenda KUYASOMA yanasomeka bado,...... na husomi hata  BIBLIA na  KORANI   ingawa unajua vina UJUMBE  MWEMA tu,...
    ....kama tu kwenye kitabu cha KAMASUTRA ubobeavyo kwenye PICHA na sio MAANDISHI kisa kwa ladha yako VITABU hivyo banangenge vimekosewa kuandikwa VIZURI katika mirindimo  ikupandishayo MDADI WA KUSOMA  kama vile yaandikwavyo MAGAZETI YA UDAKU katika mirindimo iwezayo kukufanya uone HABARI ya KHADIJA hapendi kuvaa chupi ni HABARI MUHIMU SANA kuliko habari ya KUNA MAFURIKO Ludewa. .:-(

     Swali:

    • AU? 
    • Si unakumbuka pia kuwa  UJUMBE MZURI NA WA BUSARA kwa MTU MWINGINE  inawezekana ni KILE ukiitacho wewe  MATUSI?



     Staili ya MUANDISHI wa habari,...... yaweza kusababisha usomee UANDAJI wa UDONGO walao wajawazito, HISTORI  au tu  angalau upende kujisomea stori za  UCHAWI uziogopazo,.......kisa STALI YA UANDISHI  kukufanya usiyependa kusoma uhusudu KUHAMIA mstari unaofuata katika HADITHI kisa kanogewa na SENTENSI ya kwanza ,...


    ..... kama tu kwa ASIYE PENDA UGALI WA MUHOGO kujikuta kamaliza bonge la sima kisa MBOGA tamu kusababisha tonge la kwanza kumshawishi MLENGWA kukata TONGE la pili na mpaka kumaliza MAAKULI bila kukumbuka huwa HAPENDI UGALI wa MUHOGO kwa kuwa yeye ni MUTU ile inapenda YUGALAI (Ugali kwa Kizungu) iliyopikwa kwa kutumia  UNGA WA SEMBE.:-(


    Ndio,...
    ... UGALI bila MBOGA unalika bado .:-(



    NI wazo tu HILI MHESHIMIWA!:-(

    Hebu India.Arie, Dobet Gnahore, Idan Raichel na Blue Miller walete- Palea




    Au tu India Irie na Dobet Gnahore waendelee na -Pearls


    Bila kumsahau ALI KIBA katika kibao-Mac Muga

  • HIARI IPO hata kama kwa HIARI atendwavyo MWINGINE yachokoza na kuchokonoa HURUMA YAKO kwa kuwa ANAVYONANILIWA hupendi!:-(

    Posted: February 22, 2010, 9:14 am by SIMON KITURURU




    NDIO hata ubishe ,...... katika KUNANILIU ,.......kuna WANANILIWA pia ,....... ambao  WANANANILIWA VIZURI kwa bidii TU  kwa hiari yao wenyewe.:-(


    Swali:
    • Kwani unafikiri  WATANZANIA katika kunaniliu a.k.a KUCHAGUA CCM na sio vyama vya UPINZANI unafikiri WENGI TU  hawafanyi hivyo kwa HIARI yao tu hata kama WEWE hupendi CCM Mkuu?

    • Kwani unafikiri  ni MANGAPI  utendewayo ambayo unasaidia WEWE MWENYEWE  yafanikiwe  UTENDWE VIZURI TU kwa faraja?

    Kuna yalazimishwayo,....... lakini  HATA KAMA HUPENDI haiondoi ukweli kuwa kuna  WAUMIZWAO,...... ambao yaumizayo  ni ya HIARI  KWAO.:-(

    Kuna yalazimishwayo,... ....lakini hayohayo usipostukia hasa   KAMA WAUMIZWAO NI WAJANJA  unaweza kushabikia mchokonoo UNAOUMIZA bila kujua  kwa kuwa WAJANJA  wanaweza tu kutungia jina tofauti  MCHEZO wakati KITENDO NA  maumivu  ni YALEYALE.:-(

    Swali:
    • Si unajua adhabu nyingi tu  wapewazo watu kama tu KURUKA KICHURACHURA ,  zikifanywa kwa HIARI wajanja HUZIBADILI JINA na kuziita  ni  MAZOEZI?

    • Si unajua KUBAKWA, na  MAMA WATOTO  kulazimika kuwa kiburudisho kwa baba watoto bila kuandaliwa   kwa kuwa baba watoto SAA HIYO  anataka kula mali zake alizozitolea MAHARI   ,kwa MDADA kunaweza kukawa na maumivu sawa kimwili ,  ingawa moja MDADA kabakwa MIGOMBANI na JINGINE ni  IMEBIDI KWA HIARI  mdada  avumilie MAHITAJI YA MUME WAKE kwa kutii MAFUNDISHO YA SOMI wake KWENYE UNYAGO kuhusu HIARI YA MWANAMKE ni MAAMUZI YA MUMEWE , na kwahiyo  haliitwi KUBAKA?




    NIMEACHA !
    HILI  ni WAZO tu MHESHIMIWA!Jumatatu  NJEMA!

    Au tu Jean-Claude Naimro na KASSAV wabadili tena kwa-Ave'w Doudou



    Au tu JOCELYNE BEROARD wa KASSAV alete -Kay Manman




    Au tu Jacob Desvarieux  na   KASSAV  wapoze pia zaidi kwa -Malad aw

  • SHOGA njoo pembeni TUMSENGENYE MAMA MWENYE NYUMBA kwa kuwa HAUSIGELI ni kibonde , TUTAMSUTA uso kwa USO!:-(

    Posted: February 22, 2010, 8:50 am by SIMON KITURURU
     Katika dunia yenye  WENYE mabavu,....... kwa kawaida WABABE HUSENGENYWA kwa SIRI ili wasije kubwenga MTU bure  wakisutwa USO kwa USO,....

    ....na ASUTWAYE uso kwa uso ni ambaye inaaminika katika tukio  hana MABAVU na akileta za kuleta wakati anapandishiwa sketi a.k.a ANASUTWA hata  MBATA na KONZI anawezabwengwa  kama nyongeza juu ya MSUTO.:-(




    Swali:

    • SI unakumbuka mara nyingi  HATA WEWE ufanikiwaye KUMSUTA uso kwa uso   KWA KAWAIDA ni YULE ambaye humuogopi VIZURI?

    • SI unakumbuka UMSENGENYAYE  na KUMTETA na MASHOGA ZAKO  hasa yule rafiki yako bado  ni ISHARA ya KUOGOPA KUZUNGUMZA NAYE UFIKIRIACHO  na ndio sababu INGAWA UNAMSENGENYA NA MASHOGA ZAKO WENGINE  bado KWA KUMUOGOPA una kahofu kakutotaka ajue ni wewe UMTETAYE  kisa  unajua ana mimba ya PADRE  na wala si ya HAUSIBOI kama walivyohisi   WAMBEYA wa nyumba ya jirani  waliovalia njuga ufala wa MUME wa rafikiyo kabla huja waongezea MSENGENYO kwa kuwa tonya ishu?

    • Si unakumbuka kuna WAPINZANI wengi wa Rais KIKWETE ambao ni mabingwa tu ya KUMSENGENYA na KUMTETA wakati hayupo lakini akitokea KIJIWENI kumsuta HAWAWEZI?



    Kwa mtazamo huo usishangae mahusiano YA ASUTWAYE  na ASENGENYWAYE na KUTETWA yakiwa na MWALIKO uliokaa mkawai :
    Njoo tumsute MLALAHOI,...... kwa kuwa FISADI  inabitumsengenye tu na kumteta kwa siri kwa kuwa mpaka POLISI ni hawala zake.

    Njoo tumsute, KUMTETA  na kumpiga makonzi MSENGE,...... kwa kuwa NJEMBA RIJALI yenye wake wengi hata  kuisengenya tu kwa hilo KIMILA nyingi za KIAFRIKA bado haiwezekani.

    Njoo  tumsengenye MAMA MWENYE NYUMBA na sio HAUSIGELI,........ si unajua  kumsuta MAMA MWENYE NYUMBA unaweza kuchochea kubwengwa na mpaka BABA MWENYE NYUMBA ingawa kwa kumsuta HAUSIGELI  yaweza kuonekana sawa TU  ingawa HAUSIGELI na wala sio MAMA MWENYE NYUMBA ndiye kiburudisho cha  Baba Watoto.



    Swali:
    • Lakini si unakumbuka asengenywaye kama hastukii asengenywacho  MSENGENYAJI labda anapoteza tu MUDA?
    • Si ulishawahi kufikiria kuwa mara nyingi UMSUTAYE unaweza pia kumsengenya lakini si kila UMSENGENYAYE unaubavu wa kumsuta kwa kuwa kusuta mtu huhitaji umuangalie machoni?



    Ndio,.......labda hata katika  ya  VIONGOZI wako  MAFISADI kuna uwezekano yote uyasikiayo ni MISENGENYO na kuteta tu kwa wasio na MABAVU ,.......kwa kuwa hakuna wa KUWASUTA uso kwa USO.:-(
    CHA ajabu ni kwamba,...
    ....wengi waogopwao KUSUTWA uso kwa USO mabavu yao  MISINGI YAKE  inatokana na  kitu hicho hicho ``KUOGOPWA´´.:-(
    Swali:
    • Unauhakika weye MTANZANIA  Rais Lowasa Mkapa akiwa mbele zako utaongelea Richmondi kama utetavyo kijiweni na washikaji?

    Ni wazo tu DHAIFU HILI Mheshimiwa lakini pamoja na yote NI  WAZO!



    Hebu FALLY IPUPA abadili kwa -Cadenas





    au tu tulia na Awilo Longomba - Awa Imani - African Tonic katika- C'est pas Complique


Blah blah blah

Fish cakes

Alas a fish cake.

Yet more fish cakes

Guess what ... yeah ... fish cakes.

The end of the fish cakes


Kenyan Blogs