SIMON KITURURU- MAWAZONI

  • Mkusanyiko wa KINACHOFIKIRIWA ambacho kwa sababu MTUZ zinajiheshimu HAKISEMWI.

    Posted: February 15, 2010, 11:14 am by SIMON KITURURU
     MKUSANYIKO wa VIFIKIRIWAVYO visivyotamkwa,....... labda vina siri ya MATATUZI ya YADUNIA ambayo sio siri yaonekanayo hayana MTATUZI.



    KINACHOFIKIRIWA  ambacho KWAKO ni chepesi kutamkwa,...
    ... labda sio  chepesi hivyo hata kama sio CHA KIJINGA kwa kuwa  kunauwezekano mkubwa kimepitia MCHUJO uchambuao ni YAPI MTU AYAFIKIRIAYO anataka kuyafanya  kwako iwe SIRI na aropokacho ni asilimia tu fulani la MROPOKO hata kama kwa kukuficha kitu anakucheleweshea muda wa kustukia staili ya kukaa kwako haimfai kimwana asiye vyaa kificha nyeti ambacho katika swala la kuchunguliwa ni TATUZI.



     NDIO, kwa kujiheshimu kunavisivyo tamkwa,...
    .... na matokeo yake labda ufikiriavyo ni siri wala SIO SIRI na kwa kukwepa kwako kutamka neno bado sentensi uifikiriayo isiyo na heshima yajulikana na kwa ukimya  wako na ufikiriacho NI SIRI  wala tatizo lako  la kuficha siri zako HALIPO kwa kuwa HUNA SIRI na kwa hiyo  halihitajipata ulilengalo TATUZI.

    Swali:
    • Unafikiri  kukwepa kwako kutamka baadhi ya maneno kwa kuwa UNAJIHESHIMU hakuchangii mkusanyiko wa SIRI MBOVU duniani?

    • Madhumuni ya kukwepa kwako kudakwa unashabikia TOPIKI FULANI HADHARANI au tu kukwepa kwako tu baadhi ya maneno -kama mtu, - unafikiri  hufanya ufikiriavyo SIRI kwa wakujuao kama mtu?

    • Ukimuona mjamzito hata bila kutamkiwa kwani hujui jina HALISI AMBALO HULITUMII  la KITENDO ambacho unafikiria  au KUHISI alifanya ingawa mwenye mimba ni  bonge la mpole?



    NI WAZO TU HILI MHESHIMIWA!JUMATATU NJEMA!


    Hebu Milton Nascimento arudie-Travessia



    Au tu hebu Gilberto Gil alete-Toda menina baiana




    Au tuondoke tu BRAZIL na kurudi BONGO NYOSO kupata dozi kutoka kwa USWAZI waongelee-True Love

  • Madhara ya kufikiria VITU bila SABABU,....

    Posted: February 15, 2010, 10:39 am by SIMON KITURURU
    .....  unaweza KUJIKUTA unastukia mpaka yasiyo KUHUSU.:-(

    Ingawa KUFIKIRI ni bonge la shughuli ambalo mara nyingi wala halihitaji SABABU,....... matokeo yake  MTU waweza jikuta unayapa umuhimu YASIYO na UMUHIMU kwa kuwa tu UNAMIAKILI na  katika kuitafutia shughuli wabobea katika kufikiria mpaka ya wengine na kutafuta jinsi ya kuhalalisha yasiyo kuhusu YAKUHUSU.




    Swali:
    • Unafikiri UNAFIKIRIA vya kutosha?

    • Si inasemekana kuna waliogeuka vichaa kwa KUFIKIRI?

    • Unafikiri MADHARA YA KUFIKIRI na FAIDA za KUFIKIRI kipi chema ingawa vyote vyaweza kufanikiwa kutokukupa JIBU?


    NI WAZO tu HILI Mkuu!

    Hebu binti ya ELIS REGINA ,     MARIA RITA  alete- Encantada




    Au tu MARIA RITA aendelee tu na kitu- CUPIDO



Blah blah blah

Fish cakes

Alas a fish cake.

Yet more fish cakes

Guess what ... yeah ... fish cakes.

The end of the fish cakes


Kenyan Blogs