SIMON KITURURU- MAWAZONI

  • Starehe ya KUMPIGA mgeni ili MWENYEJI apone, JIFUNZE kitu South AFRICA!

    Posted: May 19, 2008, 1:03 pm by SIMON KITURURU
    USIJIDANGANYE!
    Si kweli ukarimu wa mwenyeji wako ndio ushahidi kuwa anakukupenda au anahusudu umemtembelea chobisi.

    Nadhani inawezekana umewahi kusikia kamsemo; Mgeni njoo , MWENYEJI apone!

    Mgeni akija, kuna uwezekano yule jogoo wa krismas akachinjwa mapema, na pesa za kununulia nguruka wa kesho, zikanunua soda.

    Lakini mgeni akiendelea kuwepo, kuna watu watapata muda wakubadili mkao , kutoka mkao wa jamaa mgeni hatuwezi kumpa jembe tukaenda naye leo kulima, mpaka mkao wa ; HIVI WEWE UTAONDOKA LINI?

    Kwa walioko nchi za watu wenye rangi tofauti ni rahisi mpaka kusingizia kuwa ni ubaguzi tu wa rangi ufanyao mtu kutokukutaka kwake au hata katika choo cha jirani.

    Lakini, kuna watu hawampendi tu mgeni kutokana na sababu moja kubwa kuwa,YEYE ni MGENI.

    Binadamu tunaudhaifu wa kutoelewa vigeni.

    Lakini...
    ......Kitu kigeni tusichokielewa, tunaweza tukajikuta tu.... ...
    • Tumekiabudu kama MUNGU
    • Tumekiogopa kama Shetani
    • Tuna wasiwasi nacho kama kuonja nyama ya MBWa
    • AU KAMA KAWAIDA yetu TUTAKISINGIZIA hasa kwamba ndio SABABU ya YOTE mabaya yanayotutokea.

    Nakubali, umasikini, ujinga, na mengine mengi yanaweza kusababisha mgeni awe nishai!
    DUH!

    JIHADHARI tu kama uko SOUTH AFRICA sasa hivi na si Msauzi, unaweza kupigwa kibano.
    Jihadhari kama hauko Nchini kwako, au hata mtaani kwako, unaweza kupigwa kibano.

    Nimebanwa kidogo!
    Labda nitaendelea na topiki hii badaye kama bado iko mawazoni!
    Angalia HAPA
    au soma HAPA kama unataka kujua fununu ya yawatokeayo walio SOUTH AFRICA


    KAMA unanafasi....
    Hebu pitia kidogo UMASAINI kama kulivyorekodiwa wakati jamiii inawakarimu Familia ya GARSON(Tahadhari:Kama hupendi kuona damu au mnyama akichinjwa usiangalie!)


    Au tukatike viuno kama SOUTH AFRICA tu, ambako hatutakiwi kuwepo..katika kibao kiletwacho na TSHE-THSA BOYS
  • FURAHIA maisha kwa kupata UKIMWI.:-(

    Posted: May 19, 2008, 11:43 am by SIMON KITURURU
    Maswala ya UKIMWI si ya kutania.
    Watu mamilioni wanateseka sana hivi sasa kutokana na UKIMWI.

    Lakini....
    ...Binadamu haachi kunishangaza!

    Kuna watu kibao inasemekana huwa wanatafuta kuambukizwa UKIMWI kwa makusudi ili kufurahia maisha.

    Utasema utakalo sema, lakini , hawa watu kwa taaluma za kisasa za kumjua binadamu kwa vipimo vya kisasa, SI VICHAA.

    Hili swala ingawa watu wengi wanasema liko kwa WASENGE tu, kuna mmoja wa watafiti wa maswala haya ambaye nimewahi kuongea naye , anasema swala hili liko hata kwa binadamu wapendao kugusanisha HASI na CHANYA (heterosexuals)katika miondoko ya mikasi a.k.a Ngono.

    Tofauti kati ya Wasenge na WachezaJUMAnaROZA ni kwamba, wasenge wamefikia kuandaa pati maalumu kwa ajili ya tukio lakuwini LOTTO katika kubadili status yako kutoka negative kuwa positive, a.k.a SEROCONVERSION

    Swali:
    • Unakumbuka kuna wakati UKIMWI ulidhaniwa kuwaathiri WASENGE pekee duniani?
    • Unakumbuka kutokana na jamii kutofagilia USENGE, kuna wasenge kibao ambao hawakustui tu kuwa wako katika fani?
    Kwa WASENGE , ilikukusaidia upate UKIMWI kwa FURAHA, huwa wanaandaa pati ziitwazo BUG PARTIES.

    Katika pati hizi kunakuwa na GIFT GIVERS na BUG CHASERS.
    Hawa Gift givers ndio wenye virus tayari na BUG Chasers ndio watakao kuambukizwa.

    DUH!
    NAACHA HII TOPIKI!

    UNaweza kupata habari zaidi mtandaoni kwa kutafuta manenoo kadhaa..

    Pata basi terminology katika lugha ya KIKWERE kidogo.....
    Terminology Bugchaser(also bug chaser) An HIV- man who actively seeks HIV infectionConversion partyA sex party at which men attempt to seroconvert themselves or others (see also: bug party)Fuck of deathUnprotected sex between an HIV- and an HIV+ manGiftgiver(also gift giver; gift-giver) An HIV+ man who infects or attempts to infect willing partners with HIVGiftgiving(also gift giving; gift-giving) Infecting a willing partner with HIVThe giftHIVPozcum(also pozload, poison seed) The ejaculate of an HIV+ manNeg buttSomeone who is HIV-"Poz my neg hole"Give me HIVStealth fuckinginfecting unsuspecting sex partners with HIVUnaweza kumsoma huyu jamaa kidogo pia ,kama wewe mvivu kusaka vistori mtandaoni, akufundishe kuhusu jinsi ya kuwa MSENGE.

    DUH!

    Nilitaka kukukimbia, lakini...
    ...... nimeona nikuache tena na ELIZABETH PISANI, mtafiti wa maswala, akupe BUSARA za MALAYA ,au ajaribu tu kukushauri kuwa kama watu kwa wingi katika maeneo fulani wangefanya matusi;(samahani kwa lugha chafu!)nilitaka kusema, anadai kama WASICHANA wengi wangefanya UASHERATI a.k.a Kula Uroda a.k.a Mikasi a.k.a. Ngono kama KAKA ZAO, basi UKIMWI ungepungua duniani.

    Anadai kama uko SOUTH AFRICA, moja ya njia kubwa kwako WEWE mwanaume kujilenga upate Ukimwi ,FUNGA NDOA .

    CHeki kitabu chake
    au
    Msikilize kidogo.....


    AU...

Blah blah blah

Fish cakes

Alas a fish cake.

Yet more fish cakes

Guess what ... yeah ... fish cakes.

The end of the fish cakes


Kenyan Blogs