SIMON KITURURU- MAWAZONI

  • KATIKA kumfuatilia MASIKINI inayedaiwa ANANOGEWA zaidi KUZAA!

    Posted: May 13, 2008, 7:25 pm by SIMON KITURURU
    Jasho laweza kukutoka wakati unajaribu kutetea utajiri wa TANZANIA katika macho na masikio yaonayo jinsi gani NCHI tajiri kama TANZANIA inavyoweza kuwa na watu maskini au kuitwa nchi MASIKINI ya dunia ya tatu.

    Lakini...
    ....Yeyote awezaye kuona UTAJIRI ndani ya nchi iitwayo maskini na yenye maskini kama TANZANIA, ataweza kujua jinsi gani hata neno TAJIRI au MASIKINI liwezavyo kuwakilisha mtazamo tu fulani wa watu kutokana na jinsi tulivyofundishwa kuangalia mambo.

    Lakini...
    ....Wengi huweza kukuapia kuwa wanajua kipimo cha utajiri na umasikini hapa duniani.

    Na hata ukijifanya unatumia vipimo vya furaha au kuishi na uvitakavyo tu , bado unaweza kujikuta unachekesha katika jamii ambayo tokea unazaliwa inajaribu kukujenga kimawazo kufikiri walionavyo zaidi wamekuzidi ujanja.

    Tatizo ni kwamba,.....
    ...... jamii ina staili ya kuangalia ulivyonavyo utake usitake, na hujaribu kukutafsiri kuwa wewe kiboko au panya.

    Cha kusikitisha ni kwamba,.......
    ......ingawa umaarufu wa tajiri mara nyingi ni umaskini wake kama unachagua kumuangalia huyo tajiri bila kutishika na nyumba, magari au suruali yake ya kodrai, bado kwetu wengi tajiri ni mjanja hata akifa kwa BP au utajiri wake wa kifikira ukiwa ni KUBWA jinga.

    Swali:
    • Hivi ni kweli MASIKINI huongoza kwa kuwa na watoto wengi?
    • Nani kasema MASIKINI wananogewa ZAIDI kujifungua ZE TOTOS?
    Kati ya jambo nililoulizwa mara kadhaa hivi karibuni, ni kwanini masikini hawajifunzi kuwa ni ghali kuzaa watoto wengi.

    Ukiacha CHINA ambako kisheria huruhusiwi kuwa na watoto wengi, utastukia nchi nyingi zilivyozidi kutajirika, ndivyo asilimia kubwa zaidi ya raia wake walivyopunguza namba ya watoto katika familia.

    Kama unafikiria zaidi ughali wa kulea mtoto, unaweza kushangaa kwanini matajiri wawe na watoto wachache halafu masikini wawe na watoto wengi.
    Swali:
    • Unafikiri maana na vigezo uitavyo ni utajiri , vingekuwa na tafsiri gani kama ungelelewa katika jamii ya ujanja ni kuwa na kidogo?
    • Unauhakika utajiri si jambo liishio mawazoni tu?
    • Kisaikolojia unafikiri ni mpaka uwe na walivyonavyo matajiri ilikupata ladha tamutamu ya tamu ya kuwanavyo?


    Si mshauri masikini aige tajiri katika uvivu wa kuzaa!


    KWANI Inasemekana ni rahisi zaidi kwa maskini kufa kuliko tajiri kukata roho katika mazingira ya dunia hii ya leo ambayo ujanja ni jinsi gani unaweza kununua madawa, kujilipia hospitalini au hata kuweza kujinunulia dagaa na mchicha .



    Ila.....
    ...Tafsiri nzima ya utajiri , inaweza isiongee lugha moja ukimuuliza tajiri wa Kiafrika afuataye UAFRIKA ndani ya AFRIKA na tajiri wa KIJERUMANI, afuataye UINGEREZA aishiye ndani ya MAREKANI kuwa ;UTAJIRI ni nini?

    DUH!

    NACHOJUA......
    Umasikini noma!Hasa kutokana na kumaanisha masikini ni mtu anayeshindwa kupata atakacho.

    LAkini......
    Swali:
    • Tajiri umjuaye unafikiri anapata vyote atakavyo?
    • Unauhakika kama huvifikirii sana ulivyokosa; wewe si tajiri?
    DUH!

    UFIKIRIAYE ni masikini , si lazima kuwa kweli ni masikini, kama utajiri kwako ni jinsi mtu alivyojilimbikizia asivyohitaji.

    Halafu tukumbuke kuwa katika maswala ya vipimo, familia yenye watoto wawili ni wengi, kama walitaka kuwa na mtoto mmoja.

    PIA....
    ...Pamoja na sifa zote mbaya za umasikini, kama ushawahi kumsikiliza Mother TERESA, watu husahau ukaribu wa masikini na MUNGU.

    LAKINI kama ....
    ......kwa masikini watoto ni MTAJI , BIMA, TREKTA na hata UTAJIRI, kwanini wasizae sana?

    BASI bwana topiki imenishinda!
    Samahani hapa NAWAZA tu !

    Hebu twende KENYA tukatembelee CRIB ya OMONDI....


    Ngoja niache tusikilize utundu wa COURTNEY PINE akiwa na MANU DIBANGO katika midomo ya BATA na...au..... DUH! ..... LION OF AFRICA.
  • Nataka , HATAKI!Akiwa TAYARI au KUTAKA, nimechoka!:-(

    Posted: May 13, 2008, 6:22 pm by SIMON KITURURU
    Katika maswala ya" NATAKA, HATAKI , akiwa TAYARI nimechoka", najaribu kuangalia Mahusiano ya muda, watu na tukio litokealo , hata kama tunaweza kusingizia kuwa haya maswala ni moja ya sababu zifanyazo kuwa wewe umepata na sisi wengine tumekosa.

    Udhaifu wa kibinadamu, hauruhusu tuwepo sehemu zote au tuwepo katika nyumba wahitajiyo hausiboi au hausigeli mwenye sifa kama zetu wakati au siku wenye nyumba wasubiriyo mtu agonge hodi, akitafuta kazi.

    Ni kweli inasemekana kuwa udhaifu wa binadamu unatofautiana ukiuchungulia katika mida tofauti au maeneo tofauti.

    Kwa hiyo ,...
    ....inaweza kuwa ni kweli, ndani ya muda au siku fulani, kumtongoza HIDAYA ,anawezakukubali kirahisi kuliko wengi wahisivyo kutokana na wamjuavyo kwa sifa zake za kununia wanaume.

    Kwa hiyo,...
    .... kuna muda unaweza kujikuta umefanya dhambi kirahisi zaidi kuliko jana.

    Kwa hiyo ,....
    ......inawezekana ndani ya muda fulani, ni rahisi kuliliza jibaba zima hata bila KULIPIGA roba ,kwa kulitukana kuwa ni ;KUBWA zima jinga!

    Swali:
    • Unakumbuka kuwa labda ungecheza LOTTO sasa hivi wakati unanisoma hapa, labda ndio muda wako wa kushinda?
    • Hujawahi kushindwa kitu watu wakisifiacho kwa urahisi wake?
    Inasemekana kila mtu ana nafasi yake yakuwa milionea au kupata , kama atacheza mchezo sahihi katika dakika, sekunde au muda sahihi.

    Uhusiano wa kitu kiitwacho BAHATI NASIBU na ashindaye bahati nasibu, ni uhusiano wa mcheza sahihi katika muda sahihi na ndani ya mchezo sahihi.

    LAKINI ...
    ...Kama kila mtu angeweza kugundua siri ya kucheza sahihi , muda sahihi , ndani ya mchezo sahihi, inawezekana WATU WOTE uwajuao, WANGEKUWA WANALIA sasa hivi, na hii DUNIA yetu yenye mapungufu isingeweza kuwepo tena , kutoka na mtu kufanya kitendo sahihi kama cha kulipua mabomu ya nyukilia.

    Tukumbuke kuwa, kucheza kwako sahihi iliumpate Hidaya au Hamisi, kucheza kwako sahihi ili upate kazi fulani au mshahara fulani, kuna ambaye mchezo wake sahihi atakao kuucheza sahihi, ni kujaribu KUKUUA WEWE kutokana na rangi au sura yako, au kukuliza kutokana na afurahiavyo staili yako ya kulia.


    Sidhani kama ni kwa bahati mbaya tu DUNIA HII tuishiyo iko kama ilivyo.
    Sidhani hata binadamu wajaribu vipi ,wanaweza kuondoa mapungufu ya binadamu na dunia hii.

    Kwahiyo nafikiri....
    .. bado kuna ambao tutawaita kuwa wana bahati kutokana nakufikiri kila wakijaribu kitu fulani , wao hupata wakati siye tukimngoja HIDAYA uchochoroni, hapiti njia hiyo siku hiyo.

    SWALI:
    • Unakumbuka umpendaye anaweza akawa anampenda yule ambaye anampenda yule akupendaye ambaye humpendi?
    • Unakumbuka kuwa hapo hapo katika barabara uivukayo, KUNA MTU atagongwa au alishagongwa muda fulani?

    Katika maswala ya kukosea TIMING au kamuda, unaweza kujikuta unawaza...
    ....Ningependa kuonja sasa hivi , lakini dhambarau hazijaiva.
    ...Ningependa kuonyesha penzi, lakini mbona sina mpenzi zaidi ya hili limtu niishilonalo kwa kuogopa nini jamii itasema ndoa ikivunjika.


    Lakini.....
    ...Mpenzi wako achekaye ukimtekenya, sikushauri umtekenye ilikujaribu kumpoza au kumuondolea maumivu ya kichwa au msiba.

    Na kuna wakati kama hutaki kushindwa, ni afadhali usimpe kauli ya kutaka mkacheze MCHEZO wa BABA na MAMA au wa KUIBA yule atokaye MSIKITINI au KANISANI, wakati utaalamu wako wa kauli unashindana na wa PADRI au SHEKHE, ambaye ashamuingiza akilini umlengaye, mahusiano ya tamaa zako mbaya za kibinadamu na DHAMBI au AHERA.



    LAkini.....
    .....Nafikiri pamoja na udhaifu wa binadamu, ni rahisi kugundua kuwa ukirudiarudia mara nyingi kitendo kwa kutumia njia ujuayo ni sahihi, unaweza kujikuta UMEPATA kazi uitakayo, umepata MIMBA au umefanikiwa kufanya kitendo sahihi ndani ya muda sahihi na kweli jiwe ulilorusha jikoni kwa mtu , limempiga BABA mwenye nyumba aliyekwenda kuonja mboga kisiri jikoni wakati MAMAA anasukwa nywele kibarazani.

    Naamini kama tunajitahidi kufukuzia kitu, sekunde ijayo inaweza ikaoanisha kitendo sahihi , mahali sahihi na muda sahihi na kutuwezesha kufanikiwa lile jambo au kufa.

    AU?
    DUH!
    Samahani niko tu MAWAZONI kidogo!
    NAACHA basi!

    Mpate LUPE FIASCO katika FIGHTERS


    AUtwende tu na PEPE KALLE kumtafuta kipenzi HIDAYA

Blah blah blah

Fish cakes

Alas a fish cake.

Yet more fish cakes

Guess what ... yeah ... fish cakes.

The end of the fish cakes


Kenyan Blogs