SIMON KITURURU- MAWAZONI
-
KUKATA TAMAA ni UJANJA
Posted: May 3, 2008, 1:00 pm by SIMON KITURURU
Kuna atakaye sema kukata TAMAA ni kitu kibaya!
Lakini...
...ukikata tamaa, utajipa nafasi kuwa HURU kujitoa katika MNASO.
Kukata tamaa ni SANAA kali, si kila MTU ni stadi katika kukata tamaa kinadhifu katika swala ambalo anahisi kukata tamaa na KUCHEKESHA ni saresare maua.
Ukikata tamaa, unaweza kujikuta umeacha kuhangaikia kitu.
Ukikata tamaa , unaweza kuacha kuchamba kwa sababu tishu, maji, mchanga, majani au jiwe utumialo kama MAKOKONEO pale msalani ,vinakosa umuhimu sana kwako kutokana na mnuko wa mvundo wa chooni na MANUKATO ya UTULI, hukosa tofauti kubwa.
Ukiweza kuishi UKIWA na MATUMAINI wakati unaweza kufanya afanyacho aliyekata TAMAA, wewe unaFURAHA maishani na jirani hakutishi.
Swali:- Unakumbuka kama ushawahi kutamani inawezekana huhesabu tu ni mara ngapi ulikata tamaa?
- Unajua inawezekana kuwa kama tamaa zote si mbaya basi kukata tamaa kwingine ndio ushindi?
Wewe kama ni mtu wa dini lakini umefikia kwenda kwa mganga wa kienyeji kutafuta dawa ya MKUYATI, basi kuna maeneo unahisi kuna MATUMAINI na umekatia tamaa dini lakini bado unatafuta kuendeleza TAMAA ya KITU na sio KUIKATA.
NAAMINi....
...kila kitu kinaMPITO!
Kama unasikia UTAMU sasa hivi, USIKATE tamaa, UCHUNGU uko kwenye kona , utakudaka tu hata kama sio leo.
Kama uko kwenye MACHUNGU leo hii, kumbuka UTAMU ni kifo.Utakudaka tu, hata kama sio leo.
USIKATE TAMAA!
Swali:- Hivi inawezekana kuna UTAMU kwenye UCHUNGU?
Basi bwana NAACHA!
WIKIENDI NJEMA!
Nakuacha na KY-MANI MARLEY akikupa kibao COUNTRY JOURNEY
-
KUPAMBA maumivu kwa KUKIRI!
Posted: May 3, 2008, 12:23 pm by SIMON KITURURU
Ukikiri, unatua MZIGO wa siri na UNAANZA kutibu ugonjwa wa nyuma YA KWANINI.
Nyuma ya Kwanini kuna ile kitu yenye jina fulani lakini inawakilisha NINI kimefanyika au hakikutendeka.
DUH!
Watu hupenda kusikia kutoka kwako mwenyewe umekiri walichosikia kuwa UMETENDA.
Kusikia kutoka kwa mwingine ni CHAKULA kisichoungwa, kuna ladha fulani MTU fulani anaweza kuhisi chai imekosa chumvi .
Lakini....
...IKIWEZEKANA ,usikiri JAMBO kama unaweza.
UKikiri , unawaondolea watu fulani faida za kubunia jambo(benefit of the doubt).
Ukikiri inasemekana kuwa unatatua jambo, ingawa inawezekana unasambaza maumivu kwa mwingine kama sio wengine kwa kuwasababisha kuishi wakijua ni kweli ulijinyea kwenye harusi ya jirani.
Binadamu anajaribu sana kuondoa kero maishani mwake na ni rahisi mtu kujisahau kuwa hata ufanyeje, wewe kama binadamu, basi wewe si malaika na kwahiyo utakereka tu sehemu fulani ingawa hutaki.
Kukiri ni moja ya njia tu binadamu hujaribu kutumia kukwepa KERO moja kabla hajadakwa na KERO jingine kwa sababu umekiri.
NIsikutishe, KIRI tu kama unapata AUHENI.
Swali:- Ushastukia kila siku kuna kitu unakiri hadharani ila huiti kitendo;KUKIRI?
- Unafikiri ukikiri, UNATATUA au unabadili mchezo na kukabiliana na tatizo kwa kutumia kona nyingine?
Lakini....
......Ukifumaniwa unakula denda hata bila kukiri kuwa ulipata uroda, kuna watu watataka kujua na UKIRI kama ilikuwa chuma mboga au ulisomea umishenarini.
Lakini....
....watakao UKIRI hata wakijua, haikusaidii sana wala haiwasaidii sana kama unakumbuka dunia ilikuwepo tu kabla hujazaliwa na kufanya watakacho UKIRI .
Wanaodadisi jambo, hawataishiwa jambo la kufanya usipokiri kama bado wanataka kuwa katika uwezo wa kula na kunya(samahani, kwenda haja kubwa) kesho na kesho kutwa.
Basi bwana!
Kiri tu kama INATATUA!
Baadaye basi!
Pata tu swala kutoka kwa IMAM mtoto......akikuuliza DO YOU KNOW ALLAH?
Au pata tu Mahubiri kutoka kwa Mchungaji mtoto....
Au mshangae mpiga ngoma mtoto Kanisani......
AU msikilize tu MTOTO katika fani fulani za siku hizi.....
Blah blah blah
Fish cakes
Alas a fish cake.
Yet more fish cakes
Guess what ... yeah ... fish cakes.
The end of the fish cakes