SIMON KITURURU- MAWAZONI

  • KABLA HUJAWEKA MAUA KABURINI KWA UMFAHAMUYE.

    Posted: April 14, 2008, 11:09 am by SIMON KITURURU
    Tunakutana, kuzozana, kupendana au hata kupigana, lakini wakati kila mmoja akianza kivyake, hatuchukulii kuwa ndio inaweza kuwa mara ya mwisho kuonana.

    Hakuna ajuaye nini kitatokea sekunde ijayo, ila tunazungumzia kesho tutafanya nini.

    Hakuna awezaye yote, lakini, kila siku tunategemewa kufanya yote.

    Hakuna azikwaye na mali zake, lakini hatuachi ubahiri na kujilimbikizia.

    Tunajua hakuna ajuaye yote, lakini hatuachi kumdharau asiyejua au aitwaye mjinga.

    Swali:
    • Ushamwambia unayempenda kuwa unampenda ?
    • Ushamsamehe unayemchukia?
    • Unasubiri useme marehemu alikuwa mtu mzuri?


    Lakini....
    • Hivi marehemu lazima asamehewe?
    • Kujilazimisha kumsamehe mtu hata kama moyo hautaki, imo?

    DUH!

    USITISHIKE!

    Niko mawazoni tu!

    JUMATATU NJEMA!
    Msikilize kidogo Nina Simone akikuambia IF U KNEW

Blah blah blah

Fish cakes

Alas a fish cake.

Yet more fish cakes

Guess what ... yeah ... fish cakes.

The end of the fish cakes


Kenyan Blogs