SIMON KITURURU- MAWAZONI

  • UTAMU WA WALI na KUKU ULIOKULA JANA!

    Posted: March 23, 2008, 5:18 pm by SIMON KITURURU
    Leo ni leo!

    Ubwabwa uliokula jana hausaidii sana kukidhi mahitaji ya leo ya mlo kama una njaa ya hata kiporo cha mlenda.
    Sikukatalii kuwa jana ule wali uliokula ulikuwa mtamu kweli kama huo wali uliula.

    Lakini....
    ... kama leo tumbo halipati kitu unafikiri nikikusimulia utamu wa wali jana unamsaada sana katika kutatua swala la leo?

    Swali:
    • Umestukia hadithi za UTAMU wa pilau jana inavyonoga, kama wakati unasimuliwa leo bado umeshiba na unauhakika wa mlo?
    • Ushastukia hadithi zako za utamu wa wali uliokula jana inaweza zikawa ni adhabu masikioni mwangu kama na njaa na sina pakula leo?

    DUH!

    Nisikutishe!
    • Napenda stori za jana.
    • Nafurahia unapomsifia Nyerere , Kenyatta hata Iddi Amini kwa waliyofanya jana.
    • Napenda hata ukumbushiavyo jinsi hali ya hewa ilivyokuwa nzuri jana.
    • Napenda hadithi za wanadada na wanakaka walivyokuwa waaminifu katika mahusiano ya walioishi jana.
    • Usiseme kwa jinsi navyopenda hasa ugusiapo jinsi miziki ya jana ilivyo kuwa bomba.

    • Napenda mpaka zile nakadhalika kadhaa, zilizokuwa bomba jana.

    Sasaaaaaaaaaa........!

    Swali:
    • Mimi wa leo , utamu wa wali uliokula jana unanihusu nini?

    DUH!

    Utamu wa jana unaweza kuwa motisha ya kuongezea kautamu juu ya utamu leo.
    Utamu wa wali jana unaweza ukageuka kuwa utamu wa wali leo na kachumbari na glasi ya gongo au mbege juu yake leo.

    Lakini hadithi za utamu wa wali uliokula jana waweza ukawa ni ukatili dhidi ya masikio yangu leo mwenye njaa.

    NASIKILIZA LAKINI!
    ENDELEA KUNIPA HADITHI ZA UTAMU WA UGALI WA MUHOGO ULIOKULA JANA.

    Endeleza siku kwa kusikiliza ushahiri wa Rafael Casal

    akitukumbusha utamu wa mapenzi ya jana.


    Au turudi tu katika ZOUK na kuendelea na Jocelyne Beroad wa Kassav

  • Maswala ya Kujinyea!

    Posted: March 23, 2008, 3:52 pm by SIMON KITURURU
    Nirahisi kunyoshea mtu mwingine au kitu kingine kidole kwa swala ulilojifanyia mwenyewe.

    Lakini pia, mjanja ni lazima ajue kuwa hata kama unamnyoshea mtu au kitu kingine kidole kwa jambo lizaliwalo kutokana na kalkulesheni zako za kudaka kutolipa, ni lazima ukiri icho kitu hata kimoyo moyo kama unataka kujifunza au kutatua.

    Lakini.....!

    Maswala mengi yatutiayo matatizoni ni maswala ambayo yanaweza kumtokea binadamu yeyote.
    Tatizo ni kwamba sisi binadamu tumekuwa watumwa wa mitazamo ya jamii ifanyayo tuwe waoga kufanya chochote ambacho katika jicho la jamii kinatufanya tuonekane hatuna mpango.

    Tatizo kubwa zaidi ni kwamba, tukishaanguka katika mtazamo wa jicho la jamii , wengi wetu tunaamua kuzoea mazingira ya pale tulipoangukia.Jambo hili linatufanya tusiweze kujinasua katika makucha ya pale tulipoangukia.Hukawii kujikuta unaamua kuendelea tu kunywa gongo kama ushazoea na unajua jamii inakuita mlevi wa gongo, hata kama mbege ndio kinywaji ulichopenda kunywa hapo enzi za kale.



    Kuhusu maswala ya kujinyea......

    DUH!
    Kwenda haja kubwa kuna starehe zake!(Samahani , nilikuwa namaaninsha kujinyea.)
    Kuna watu husahau kuwa moja ya jambo ulifanyalo mapema baada ya kuzaliwa ni kujinyea.

    Lakini....

    ... hili ni jambo ambalo jamii itaendelea kukufunza tokea uanze kuelewa mambo mpaka utakapo zeeka kuwa, ni noma kujinyea.

    Kwa bahati mbaya ni kwamba, jamii haiachi mpaka ufe kukukumbusha kuwa kujinyea ni jambo la kukutia aibu na ni jambo la kuwanyea wale wakuhusuo.

    Swali:
    • Hivi unakumbuka ma astronauti waondokapo kwenda anga za juu na waingiapo tena duniani huvaa nepi ili kuwaruhusu wajinyee kistaarabu?

    Nadhani unamkumbuka huyu Lisa Novak na alivyodakwa akiwa na nepi yake katika harakati za kumfukuzia mpenzi wa mpenzi wake?


    DUH!

    Hili swala la kunyewa pia......!

    Mara nyingi watu hawataki ujinyee ili kuogopa wao wenyewe kunyewa kiaina na myo wako.

    Mambo ufanyayo yanaweza kumdhuru mtu mwingine akuhusuyo bila wewe kunuia kufanya hivyo.

    Kwa mfano ; kama wewe unafuatilia uchaguzi wa Uraisi Marekani , utakuwa umeshuhudia jinsi gani akina Obama, Clinton na.... inabidi wajitete sana kutunza uhalali wao katika uchaguzi kwa makosa ya watu wengine wawahusuo.

    Unaweza ukajikuta unadanganya kuwa wewe ni nani kutokana tu na kukwepa kuunganishwa na mnyo wa mtu , vitu , hata...... ambavyo jamii inafikiri vimejinyea.



    Sasaaa!

    Unajua tena mimi na wewe si malaika na tuko katika jamii hii ambayo haiachi kutukumbusha tusijinyee.

    SWALI:
    • Unakumbuka mimi na wewe ndio jamii?
    • Wewe ni mnyosheaji vidole eeh?

    Basi ngojea na mimi nijaribu kukumbusha kitu ambacho najua kwa njia moja au nyingine ni ngumu kufanikiwa;
    USIJINYEE!

    Jumapili Njema!

    Nakuacha na Sheryl Crow

    akikupa kibao LOVE is FREE


Blah blah blah

Fish cakes

Alas a fish cake.

Yet more fish cakes

Guess what ... yeah ... fish cakes.

The end of the fish cakes


Kenyan Blogs