SIMON KITURURU- MAWAZONI
-
FASHENI ZA MAKABURI!
Posted: March 13, 2008, 8:43 am by SIMON KITURURU
Kuongelea kifo ni mwiko kwa watu lukuki.
Kuongelea makaburi kwa wengine ni swala la nuksi.
Kupita makaburini , kwa wengine ni kwa mwendo wa kama umebanwa uharisho.
Sasaaaa....
DUH!
Nahisi umestukia nafikiria sana mambo ya kifo!
Samahani!
Lakini tuendeleee........
Swala la kuchagua uzikwe wapi limenikuna kidogo tena baada ya kukutana na namba zisemazo:- Asilimia 50 ya Waingereza wanataka wachomwe na majivu kutupwa maeneo baada ya kufa.
- Asili mia 40 ya Wamarekani (USA) wanataka wachomwe na majivu kutupwa vilevile.
Lakini....
Kilichonizingua zaidi ni huu mradi wa PIRAMIDI MPYA , ambao na wewe unaweza kushiriki kujiandaa kuzikwa kwenye PIRAMIDI lililoko katika hatua za kuanza kujengwa.
Kama unataka kuzikwa kwenye piramidi hili, BBC inaripoti kuwa bei ya jiwe ni EURO 700 kwa bei ya sasa.
DUH!
Sasaaa......
Swali:- Hivi makaburi umuhimu wake haswa ni nini?
Naamini kuna wengi ambao hutembelea makaburi ili kuendelea kuungana na wapendwa waliotutoka .
Wengi hutembelea makaburi ilikujiliwaza, kutoa heshima na hata kuendeleza uhusiano na wapendwa waliotutoka.
Kwa kweli kuna sababu nyingi sana zilizomfanya binadamu fulani aamue kuwe na kaburi likumbukwalo .
Lakini......
Kuna mtu kaniambia kuwa, kutokana na technolijia, watu wana video, picha na njia nyingi tu juu ya kumbukumbu walizonazo mukichwa ambazo zinaondoa umuhimu wa mtu kuwa na kaburi.
Swali:- Je kumbukumbu mukichwa ya waliotutangulia +video+picha=hatuitaji kuzika tena?
- Unaogopa kufa eeh?
- Unakumbuka enzi fulani za kale , ilikuwa mtu akifa wanamkimbia na kuhamia pengine?
- Unafikiriaje kuhusu huu mradi unaohasisiwa Ujerumani wa Piramidi ambao utachukua mtu milioni baadaya kufa?
SAMAHANI!
HABARI ZA KIFO SI ZA UTANI!
DUH!
MUNGU awapumzishe na kuwapa raha wale wote waliotutangulia mahali pema peponi!
Ngoja nikutoe katika habari hii ya makaburi kwa kukusikilizisha huyu mwana mama kutoka MALI aitwaye Oumou Sangare
SIKU NJEMA! -
Kama YESU na MTUME wakuwa na MAADUI, KAWAWA je?
Posted: March 13, 2008, 8:07 am by SIMON KITURURU
Uhuru wa kusema /kutoa maoni/kujieleza, unamazingaombwe yake.
Ukiruhusu watu wakuambie wanakufikiriaje, watakuambia mpaka yale mambo ambayo yanakutekenya sikio.
Hukawii kusikia:- Mimi nalichukia tu lile jamaa.
- Mdau kwa kupenda misifa , hata mbwa hawamfikii.
- Mtoto mzuri huyo!Ukimbishia , atakwambia kwa sababu wewe hujamuona ziro distansi.
- Jamaa kwa kupenda ubwabwa huyo!
Swali:- Kama mtembeleaji blogu nyingi, umeshastukia hata habari nzuri kuna mtu atakuja na kuitukania?
Kweli binadamu tofauti!
Mwingine matatizo ni kitu kimpacho nguvu kutatua na kwenda mbele wakati kwa mwingine ni kitu kimdhoofishacho na kumfanya asikie kufakufa.
Kweli binadamu tofauti!
Yule umpendaye , kwa mwingine ni adui kutokana na yaleyale yaliyokufanya umpende.
Mpaka dini kadhaa hazikawii kukufunza uwapende kila mtu, lakini zinakukumbusha jinsi gani wasiofuata dini yako walivyo watu nishai.
Zinakufunza umpende aliye kama wewe, na yule mwingine asiye kama wewe, unashauri ujaribu kumfanya awe kama wewe kabla hujampenda kinamna.
DUH!
Sijui kama watu kibao wamefanikiwa kuwapenda wote walioko ndani ya dini moja.
Swali:- Ushawahi kumchukia mtu bila sababu na kukiri unamchukia tu?
- Ushawahi kujikuta kuwa yule uliye kuwa unahisi ni rafiki kumbe ndio adui?
DUH!
Inasemekana kuwa, hii hali ya kujaribu kueneza upendo duniani ni alinacha fulani kutokana na necha ya binadamu.
Inasemekana binadamu watachukiana ili wajue kupenda ni nini.
Swali:- Bila chuki , upendo ni nini?
- Bila maadui, marafiki ni akina nani?
Lakini....
Mimi naamini katika upendo.
Na kaudhaifu kakupendapenda kirahisi.
MAADUI eeh!Si mnajua tunaweza kupendana kama kale kakitu kasababishako tuchukiane kakiwekwa pembeni!
Samahani lakini kwa niliowakosea!
AU?
Naacha basi kukuzingua!
SIKU NJEMA!
Tulia na Brian Mcknight
Blah blah blah
Fish cakes
Alas a fish cake.
Yet more fish cakes
Guess what ... yeah ... fish cakes.
The end of the fish cakes